Na Saida Issa,Dodoma
SERIKALI kupitia Bodi ya Maji ya Bonde la Wami Ruvu imesema kuwa imejipanga kuhakikisha inamaliza changamoto ya tatizo la maji katika mikoa...
By Mohamed Hakim
THE introduction of the Zanzibar Woman of the Year Award expresses how Non- Governmental Organizations (NGOs) support the government’s agenda of women...
NA ASIA MWALIM
LICHA ya Serikali kuanzisha mradi wa kurejesha madarasani watoto walioacha skuli, bado kundi kubwa la watoto wapo mitaani wakizurura ovyo na wengine...
Gianluca Scamacca
KLABU ya Paris Saint-Germain imekubaliana masharti na Skriniar pamoja na kiungo wa kati wa Lille na Ureno, Renato Sanchez (24) na mshambuliaji wa...
NA MWANDISHI WETU
MABADILIKO katika sehemu yoyote ile ni muhimu sana iwe kwa Serikali, taasisi ya umma ama ya binafsi au wakati mwengine hata nyumbani.
Kwa...
NA ASIA MWALIM
LICHA ya Serikali kuanzisha mradi wa kurejesha madarasani watoto walioacha skuli, bado kundi kubwa la watoto wapo mitaani wakizurura ovyo na wengine...
SEKTA ya utalii ni sekta muhimu sana ambayo inachangia kwa kiasi kikubwa pato la taifa kwa uchumi wa Zanzibar.
Sekta hiyo ni miongoni mwa rasilimali...
ILI nchi yoyote duniani iweze kufikia malengo ya kimaendeleo, haina budi kuwa na mipango bora katika matumizi ya rasilimali zake, ili kuhakikisha zinakuwa endelevu...
BIASHARA huria ni suala lililotiliwa mkazo kwa kuwa kila mmoja aweze namna ya kujitafuta riziki ya halali.
Aidha serikali daima imekuwa ikisisitiza wafanyabiashara kulipa kodi...
WATOTO ni hazina muhimu kwa maisha kila siku. Hazina hiyo kamwe haitoweza kuwa muhimu endapo haitoandaliwa vizuri sambamba, kulindwa na kupewa hifadhi dhidi pingamizi...
KWA miezi kadhaa sasa waumini wa dini ya kiislamu hapa Zanzibar wamo kwenye matayarisho ya kuelekea nchini Saudi Arabia katika miji mitukufu ya Makka...
MPIRA wa magongo ni miongoni mwa michezo mizuri ambayo miaka ya nyuma iliwahi kutamba na kuiletea sifa nzuri Zanzibar ndani na nje ya nchi.
Sambamba...
MICHUANO ya Soka ya Wanawake ya Chalenji Afrika Mashariki na Kati, tayari yameanza kutimua vumbi nchini Uganda, ikiyashirikisha mataifa manane ya ukanda huu.
Mataifa hayo...
Uislamu unasisitiza umoja, mshikamano
KUR'AN tukufu inatutaka waislamu tuwe wamoja na inatukataza tusifarikiane, kama ilivyoeleza, "Na kwa yakini huu umma wenu ni umma mmoja na...
NA ASIA MWALIM
LICHA ya Serikali kuanzisha mradi wa kurejesha madarasani watoto walioacha skuli, bado kundi kubwa la watoto wapo mitaani wakizurura ovyo na wengine...
DUBAI, UAE
DANUBE Hospitality, the one-stop, end-to-end solution provider for hospitality businesses for the Middle East is paving the way towards sustainability with its multi...
NA ASIA MWALIM
KWA miaka ya hivi karibuni kesi za ukatili na udhalilishaji wa kijinsia kwa wanawake na watoto zimeongezeka ikilinganishwa na kipindi kilichopita.
Matukio ya...
Wasifia uwepo wa maonesho hayo, Wasema yamekuwa na tija kwao
NA KHAMISUU ABDALLAH
TAMASHA la 44 la kimataifa la biashara maarufu kwa jina la sabasaba limemalizika
hivi karibuni katika viwanja vya Mwalimu Nyerere jijini Dar- es Salaam huku
likiendelea kuacha sifa nyingi zenye mafanikio kwa washiriki na wananchi waliotembelea
kwenye mabanda mbalimbali.
Washiriki katika tamasha hilo wakiwemo wajasiriamali na wafanyabiashara
wadogo walilisifia na kuona umuhimu ulivyowatangaza kimataifa hasa kwa bidhaa zao
mbali mbali hivyo kutoa fursa ya kujuana kati yao.
Mbali na wajasiriamali pia tasisi mbalimbali za serikali kutoka Tanzania
bara na Zanzibar zilipata fursa ya kushiriki tamasha hilo huku wengi wao
wakisema ni moja ya kudumisha Muungano uliopo kati ya nchi hizo mbili.
Mbali na kujitangaza pia washiriki waliieleza makala hii kwamba tamasha
la 44 la biashara kwao lilikua jukwaa lililowaongezea ujuzi na uweledi wa
kujifunza mbinu kadhaa za uchumi na biashara, kubadilishana uzoefu wa kiuchumi
na kukuza miaya ya biashara zao kati yao na taasisi mbalimbali za umma na
binafsi.
Moja ya taasisi iliyopata mwamko mkubwa katika tamasha hilo la biashara
ni Bodi ya Mapato Zanzibar (ZRB) ambapo ushiriki wake ni mara ya pili kwenye maonesho
hayo yaliyoanzishwa mwaka 1976 ambayo ilipata fursa ya kuelimisha watanzania utofauti
wa ukusanyaji wa mapato kati ya bodi hiyo na TRA.
Wengi wa washiriki waliofika katika banda hilo walikuwa wakiiuliza
maswali juu ya utozwaji wa kodi mara mbili ikiwemo ZRB na TRA.
Akizungumza na mwandishi wa makala haya, Ofisa Uhusiano wa Bodi hiyo, Badria
Attai Masoud, anasema ushiriki wa maonesho hayo umewapa fursa ya kujitangaza
zaidi.
Anasema tokea kuanza kwa maonesho hayo zaidi ya wananchi 500 wametembelea
banda hilo na kupata elimu juu ya kazi zinazofanywa na bodi hiyo.
Akielezea sababu ya ZRB kuamua kushiriki maonesho hayo, anasema maonesho hayo yanahusisha pande mbili za Muungano na wapo wananchi wanaoishi Tanzania bara na kufanya biashara zao Zanzibar na wanaoishi Tanzania bara wanaofanya biashara Zanzibar