WAPENZI wasomaji wetu wa gazeti hili pendwa, kwanza niseme Balakat el eid, nawatakia sikukuu njema waislamu wote waliomaliza kufunga mfungo wa mwezi mtukufu wa Ramadhan.

Ijumaa ijayo ni sikukuu ya eid el Hajj (Eid El adhaa) ambapo waislamu wote duniani wanasherehekea kumaliza kwa ibada ya hijja inayotarajiwa kukamilika wiki hiyo huko Makka nchini Saudi Arabia.

Hivyo basi waislamu kwa kawaida hutayarisha milo muhimu na adimu kwa ajili ya siku hiyo.

Basi katika safu yetu hii ya maakuli nimewatayarishia pishi pambe la mchana yaani Biriani ya kuku.

Upishi huu ili kukamilika ni lazima uwe na vifaa na vipimo, namna ya kupika na mahitaji ya chakula hichi kwa ujumla wake.

VIPIMO NAMNA YA KUMPIKA KUKU

Mrowanishe kuku na viungo hivi kwa muda mdogo tu

Kuku (Mkate kate Vipande) – 4  LB

Kitunguu saumu(thomu/galic) na Tangawizi – 2 Vijiko vya supu

Chumvi – kiasi

Pilipili nyekundu ya unga – 1 Kijiko cha supu

Bizari ya manjano (Haldi au Tumeric) – 1 Kijiko cha chai

Bizari ya pilau ya powder (Jeera) – 1 Kijiko cha chai

Gilgilani powder (Dania) – 1 Kijiko cha chai

Ndimu – 1 Kijiko cha supu

MCHELE NA VITU VYA MASALA

Mchele (Basmati mzuri) (rowanisha) – vikombe 7 

Mafuta ya kupikia – kiasi

Vitunguu Vilivyokatwa – 8

Tungule iliyokatwa katwa – 3

Kitunguu saumu(thomu/galic) na Tangawizi – 1 Kijiko cha supu

Pilau Masala -1 Kijiko cha supu

Hiliki powder – ½ Kijiko cha chai

Tomatoe paste – 1 Kijiko cha supu

Pilipili mbichi zipasue katikati – 4

Chumvi – kiasi

Mtindi – 4 Vijiko vya supu

Kotmiri iliokatwa (Chopped) – ½ Kikombe

Mafuta ya kunyunyuzia katika wali – 3 Vijiko vya supu

Zaafarani au rangi ya biriani – kiasi

NAMNA YA KUTAARISHA NA KUPIKA

Weka kuku aliyerowanishwa na viungo vyake katika Foil tray au chombo chocote utakachomwagia wali humo humo na kupikia biriani, kisha mchome mpaka awive na awe mkavu kiasi.

Wakati kuku anapikika, kaanga vitunguu katika karai au sufuria mpaka viwe brown na epua nusu yake weka kando.

Punguza mafuta yabakie kiasi tu, ongeza Thomu na tangawizi, na viungo vyote vya hapo juu isipokuwa Mtindi na kotmiri, endelea kukaanga hadi tomatoe zilainike. 

Ongeza chumvi, malizia mwisho kwa kutia mtindi, kotmiri na vile vitunguu ulivyoweka kando.  Masala yako tayari.

Mwagia masala juu ya kuku uliyekwishmpika changanya vizuri.

NAMNA YA KUPIKA WALI WA BIRIYAN

Chemsha Mchele uwive nusu, chuja na mwagia juu ya masala.

Nyunyiza mafuta kidogo juu ya mchele na zaafarani au rangi ya biriani.

Weka katika moto wa 350 – 400 kwa muda wa dakika 15 – 20.  Biriyani imekuwa tayari kuliwa.

VIDOKEZO UKIPENDA 

Mtindi wa kutolea Biriyani:

Mtindi – 1 kikombe

Pilipili mbichi – 1 ndogo

Kitunguu saumu(/galic) thomu – chembe mbili

Nanaa – kiasi

Chumvi – chembe tu

Weka kwenye Blender na uchanganye, kisha mimina katika bakuli