NA NASRA MANZI

WAZIRI  wa Fedha na Mipango Zanzibar  Balozi Mohamed Ramia Abdiwawa amesema Serikali itahakikisha inaendeleza ujenzi wa miradi ya kimaendeleo katika maeneo tofauti ya mji wa Zanzibar ili kukuza uchumi wa nchi .

Akizungumza katika ziara ya kutembelea miradi ya maendeleo iliyopo  eneo la Kwahani  na Kisonge alisema katika kufanikisha hilo Serikali inatayajia kujenga mji mpya katika shehia ya Chumbuni, Miembeni na Vikokotoni, ili wananchi waweze kupata makaazi bora.

Pia  alisema lengo la Serikali kuhakikisha Zanzibar inakuwa na majengo ya kisasa na yenye kuvutia pamoja na Serikali kuongeza vitega uchumi.

Hata hivyo, Waziri Ramia alitembelea  miradi ya maendeleo iliyopo kisonge na kuwataka wakandarasi wa ujenzi huo kuhakikisha miradi hiyo inamalizika kwa wakati kabla ya kumalizika kwa awamu ya saba.

“Tumepiga hatua  na awamu ya saba imefanya kazi  kubwa katika miradi yetu ni vyema kumalizika kwa wakati  awamu zijazo kuiendeleza “ alisema

Mwenyekiti wa Bodi ya wadhamini Mfuko wa ZSSF, Suleiman Rashid Mohamed alisema miradi hiyo itasaidia katika maeneo yatakayotumika kuongezeka kwa uchumi na kupata maendeleo.

Mshauri Elekezi wa Kampuni ya ujenzi wa nyumba za maendeleo ya mji mpya wa  Kwahani Adrian Eradius, alisema          miongoni mwa matatizo yanayowakabili katika kutekeleza mradi  kutofika kwa baadhi ya vifaa walivyoagiza kutokana na kuwepo kwa maradhi ya corona.