JADON SANCHO

BORUSSIA DORTMUND haitakubali kitta cha chini ya euros milioni 130 pauni milioni 116 kwa winga wa England Jadon Sancho, 20, ambaye anaripotiwa kutakiwa na Manchester United. (Westdeutsche Allgemeine Zeitung, via Manchester Evening News)

KALIDOU KOULIBALY

BEKI wa kati wa Senegal  Kalidou Koulibaly, 29, amesema anamaliza mkataba wake na  Napoli, licha ya kudaiwa kutakiwa na Liverpool, Manchester City, Manchester United na Real Madrid. (La Gazzetta dello Sport – in Italian)

NEYMAR

BARCELONA inajaribu kusaka saini ya mshambuliaji wa Paris St-Germain na Brazil Neymar, 28, kurudi tena Nou Camp msimu huu . (Marca)

LUKA JOVIC

LEICESTER inataka kumsaini mshambuliaji wa Serbia  Luka Jovic, 22,  kutoka Real Madrid kwa pauni milioni 31 kuungana na shwahiba wake Jamie Vardy msimu ujao. (Mail on Sunday)

STEVEN GERRARD

TIMU ya daraja la ya Bristol City inamtaka bosi wa Rangers Steven Gerrard kuchukua nafasi ya kocha aliyefukuzwa Lee Johnson. (Sunday Express)

THIAGO ALCANTARA,

JUVENTUS na Manchester City zimeungana na Liverpool katika harakati za kumsaini kiungo wa  Bayern Munich na Hispania Thiago Alcantara, 29. (Tuttomercatoweb – in Italian)

JONATHAN IKONE

CHELSEA na Inter Milan zimeanza mazungumzo na Lille juu ya uwezekano wa kumsajili mshambuliaji kutoka Ufaransa Jonathan Ikone, 22. (Le 10 Sport – in French)

JAMES RODRIGUEZ

BOSI wa Real Madrid  Zinedine Zidane amesema hana uhakika kama kiungo mshambuliaji wa  Colombia James Rodriguez, 28, ataendelea kubaki klabuni hapo. (AS)

NICOLO ZANIOLO

JUVENTUS na Inter Milan zote zinamtaka kiungo mshambuliaji wa Roma na Itali  Nicolo Zaniolo, 21,msimu huu. (Tuttosport – in Italian)