MASON GREENWOOD

MSHAMBULIAJI Manchester United Mason Greenwood kutoka Uingereza, 18 atakuwa na mpango mpya wenye thamani ya pauni 40,000 kwa wiki – miezi tisa tu baada ya kusaini mkapab mpya. (Sun on Sunday)

JOHN TERRY

KOCHA Msaidizi wa Aston Villa John Terry  anafikiriwa na Bristol City kuwa meneja wao mpya baada ya chaguo la kwanza Steven Gerrard kukataa kujiunga nao (Sunday Express)

JOELSON FERNANDES

ARSENAL wako tayari kutoa kitita cha pauni milioni  40 kwa mshambuliaji kutoka Lisbon Ureno U- 17 Joelson Fernandes,  ambaye pia Barcelona  na Juventus zote zinavutiwa na mchezaji huyo. (A Bola – in Portuguese)

CHRIS WILDER

BOSI wa Sheffield United Chris Wilder amesema kusajiliwa kipa Wes Foderingham, 29, haina maana kuwa Dean Henderson ataondoka klabuni hapo nabado ana matumaini  ya kubakia ambaye abnacheza kwa mkopo kutoka Manchester United kwa msimu mwengine. (Mail on Sunday)

HENDERSON

CHELSEA bado hawajaamua kuendelea kubaki aua kaucahana na Henderson. (Sunday Express)

ANGUS KINNEAR

MTENDAJI mkuu wa Leeds Angus Kinnear anasema wamiliki wa klabu hiyo watakutana na meneja Marcelo Bielsa wiki ijayo, kujadili mkataba mpya na kufanya kazi kwa lengo la kujua masauala ya uhamisho, kwenye ligi kuu msimu ujao. (Sunday Express)

DEJAN LOVREN,

ZENIT ST PETERSBURG wako tayari kutoa karibu pauni milioni 9 kwa mlinzi wa Liverpool Dejan Lovren, 31, lakini mabingwa hao wa Uingereza wanaweza kudai karibu pauni milioni 15 kwa mchezaji huyo wa  kimataifa wa Croatia.(Mail on Sunday)

SANTI CAZORLA

VILLARREAL ilithibitisha Santi Cazorla amekataa kuongeza chagua kutokuongeza mkataba wake na klabu hiyo, huku kukiwa na uvumi wa kiungo wa Uhispania, 35, angeweza kurudi Arsenal kufundisha. (Sunday Mirror)

JADON SANCHO

BORUSSIA DORTMUND wameweka kitita cha bei ya pauni milioni 115 kwa Jadon Sancho, 20, lakini mchezaji huyo wa England, anayehusishwa kujiunga na Manchester United, amekataa kuondoka katika  klabuni hiyo ya Ujerumani.

(Sunday Express)