NA MWANDISHI WETU
IKIWA waislamu kote ulimwenguni wako
katika shamrashamra ya kuusherehekea mwaka mpya wa kiislamu 1442, ni vyema kwa
muislamu ajue lini mwaka huu ulianza na kwa nini uliitwa mwaka wa hijra.
Kabla ya hijra (Mtume kuhama kutoka Makka kwenda Madina) waislamu walikua
wakijua tarekhe zao kupitia kuzaliwa kwa Mtume mfano, Sayyidina Uthman alizaliwa
mwaka wa 6 baada ya kuzaliwa Mtume baada ya mMume kupewa utume
wakaanza kuhesabu tarekhe kwa kutimilizwa kwake ambapo Sayyidina Omar
alisilimu mwaka wa 5 baada ya Mtume kutimilizwa.
Na kabla ya hapo walikuwa wakizijua tarekhe kwa kutumia mwaka wa miladia yaani
tangu kuzaliwa Nabii Issa (A.S), Nabii Mohammad alizaliwa mwaka 571M
tangu kuzaliwa Nabii Issa (A.S).
Ama miezi hii ya muandamo muhrram mpaka dhul hijja, hii ilikuwepo toka Mwenyezi
Mungu alipoumba mbingu na ardhi na idadi yake kama Qur’an inavyotueleza
ni 12 (qur’an 9:36).
Ila tu haikujulikana kama sasa tuko
mwaka wa ngapi na ndiyo maana ikajulika tu kihistoria kwamba
Mtume alizaliwa mwezi wa Rabi’unil aw wal (mfunguo sita) ambao
ni mwezi wa tatu kwa utaratibu wa kalenda ya kiislamu kama
tutakavyoona.
Mwezi wa kwanza ni muhar ram, wa pili ni swafar wa tatu ni Rabi’unil aw
wal, wa nne ni Rabi’unith thaani, wa tano ni Jumaadal ulaa, wa sita ni
Jumaadath thaania, wa saba ni Rajab, wa nane ni Sha’aban, wa tisa ni Ramadhani,
wa kumi ni Shaw waal, wa kumi na moja ni Dhul qi’da, na wa kumi na mbili ni
Dhul hujjah.
Mtume alizaliwa katika mji wa Makka tarekhe
12/3 (mfunguo sita) siku 50 baada ya tukio la kuangamizwa Abraha (al
ashram) pamoja na Jeshi lake (watu wa tembo) ambao tangu kuzaliwa Nabii Issa (A.S)
ulikuwa ni mwaka wa 571 miladia.
Aliishi Makka Mtume (
baada ya kupewa utume akiwa na umri wa miaka 40) kwa muda wa miaka 13
kisha akaamrishwa kuhamia Yathrib ambayo baadaye na mpaka sasa inaitwa al
madinatul munaw wara.
Baada ya kuhamia Madina Mtume aliishi kwa muda wa miaka 10
kisha akafariki dunia ikiwa bado waislamu hawajawa na hesabu ya mwaka huu wa
kiisilamu.
Hivyo basi, ulipofika mwaka wa 17H katika khilafa ya Sayyidina Omar ndipo fikra za tarekhe zikaanza.