KÓPAVOGUR, Iceland.

WACHEZAJI vijana wa timu ya taifa ya England Phil Foden  na Mason Greenwood hawakusafiri na timu  kwenda Denmark, baada ya picha zilizoibuka za wawili hao kudaiwa kuingiza wanawake  kwenye hoteli ya timu huko Iceland.

Wawili hao waliitwa kwenye timu ya wakubwa iliyoishinda Iceland Jumamosi.Wachezaji wamepewa miongozo madhubuti kuhakikisha wanakuwa salama na Covid – 19, na picha – zilizochapishwa na duka la Icelandic outlet DV, zinawaonyesha Foden na Greenwood wamepuuza hatua hizo.

Kitendo hicho cha kuingiza wanawake katika kambi  ni ukiukwaji wa sheria na katiba za FA kwa wachezaji wakati wakiwa katika jukumu la timu ya taifa.

Taarifa zaidi zinaeleza kuwa Foden  na Greenwood walionekana wamevalia fulana mpya za mazoezi za England na wachezaji hao hivi sasa suala lao linajadiliwa na uongozi.

Msichana mwingine alidai kuwa amewajulisha nyota wa England kuwa picha hizo zilikuwa zinasambazwa na ujumbe wa Snapchat, lakini ‘hawajazifungua’.