Ousmane Dembele

MANCHESTER United wapo kwenye mazungumzo ya kumsajili mshambuliaji wa Ufaransa, Ousmane Dembele (23), kutoka Barcelona. (Daily Record)

Dele Ali

KLABU ya Paris St-Germain wana uhakika kwamba kiungo wa Tottenham Hotspurs na England, Dele Alli (24), anataka kujiunga na miamba hiyo kwa mkopo wa msimu mzima. (Mail).

Max Aarons


BEKI wa Norwich City Muingereza, Max Aarons (20) amekubali mkataba wa miaka mitano kujiunga na Barcelona. (Sport).

Matteo Guendouzi

KIUNGO wa Arsenal na Ufaransa, Matteo Guendouzi (21), ameomba kuondoka klabuni hapo. (Tribal Football).

Arkadiusz Milik


KLABU ya Newcastle United wanamtaka mshambuliaji wa Napoli na Poland, Arkadiusz Milik (26). (Corriere dello Sport).

Tom Davies

Southampton wako kwenye mazungumzo ya kumsajili kiungo wa kati raia wa England, Tom Davies kutoka Everton. (Talksport).

Houssem Aouar

ARSENAL imepata mpinzani wa klabu inayoshiriki ligi ya mabingwa Ulaya, katika mbio zake za kumwania kiungo wa Lyon na Ufaransa, Houssem Aouar (22). (Telegraph).

Sergio Romero


MLINDA mlango wa Argentina, Sergio Romero (33), anataka kuondoka Manchester United. (Sun).

Antonio Rudiger


MLINZI wa Chelsea Mjerumani, Antonio Rudiger (27), anaangalia hatma yake klabuni hapo baada ya kuachwa kwenye kikosi cha kwanza. (Sky Sports).

Jonathan Tah

BEKI wa Bayer Leverkusen, Mjerumani Jonathan Tah (24), hayuko kwenye orodha muhimu ya wachezaji wanaowaniwa na Leicester City.(Kicker).

Ademola Lookman

FULHAM wanajaribu kumsajili kwa mkopo winga wa zamani wa Everton na Charlton, Ademola Lookman. Muingereza huyo mwenye umri wa miaka 22 kwa sasa anachezea RB Leipzig. (Evening Standard).

Jesse Lingard

KIUNGO wa Manchester United na England, Jesse Lingard (27), hatajiunga na Tottenham licha ya kuhusishwa kwake kutaka kuhamia timu hiyo. (Athleti).

Sofiane Boufal

WINGA wa Southampton raia wa Morocco, Sofiane Boufal (27), anawaniwa na klabu ya Ufaransa ya Angers. (L’Equipe).