NA MWANDISHI  WETU

MJUMBE  wa NEC ya Chama cha Mapinduzi,  Mwita  Haji Ali, amemtaka Naibu  Kiongozi  wa ACT  Wazalendo, Juma Duni Haji kutaja sera za chama chake , kwa kuhimiza ustawi wa umoja , Amani na kuacha siasa za kubaguzi.

Amemueleza hakuna kigezo kwa mgombea urais lazima  achaguliwa Mtwara, Pemba Kaskazini , Unguja Kusini au Mwanza  kama anavyodai wagombea  wa CCM Zanzibar  huchaguliwa Dodoma.

Hayo yametamkwa jana huko Makunduchi na Mjumbe  huyo ambaye alisema hoja hiyo haina msingi kuwaaminisha wananchi kwani hata Mgombea Urais wa ACT Wazalendo Maalim Seif toka tokea mwaka 1995  amekuwa akichaguliwa   jijini Dar es Salaam.

Mwita alisema  Duni anekosa werevu pia hama ubavu  na  uwezo  wa kubadili lolote lilipangwa na CCM,  na madai anayoyatoa katika kampeni zake hayana ukweli kwa kudai Zanzibar imemezwa na anawapotosha  wananchi. 

“Duni ajenge hoja na kutaja  sera za ACT Wazalendo aache porojo  na kulialia majukwani tokea mwaka 1995  hata chama chao huitisha mikutano Tanzania Bara hata mwaka huu wagombea wao wamepitishwa  mlimani City kwanini aishangae CCM  vikao vyake kuitisha   Dodoma” Alihoji Mwita.