NA JOSEPH NGILISHO, ARUSHA
TUME ya uchaguzi nchini imewaonya wagombea wanaojitangaza kwa wananchi kuwa tayari wameshashinda katika uchaguzi huu wakati Bado uchaguzi haujafanyika na hivyo kuleta taharuki kwa wananchi ambao ndio wapiga kura.
Akizungumza jana jijini Arusha Mkurugenzi wa Tume ya Uchaguzi nchini NEC, Dk. Charles Mahera, amesema kuwa tume ya uchaguzi ndio yenye mamlaka kisheria ya kutangaza matokeo ya uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani na siku ya uchaguzi bado hivyo Tume imewaonya wagombea kuacha kupotosha watanzania na kuwajengea taswira kuwa wamekwisha shinda .
Amesema kitendo hicho ni kibaya kwani kunakuwa na malengo ya kuvuruga amani kwa watanzania na nikinyume na taratibu za sheria hivyo kitendo kinachofanywa na baadhi ya wagombea kwa kuikashifu tume ya uchaguzi kuwa itaiba kura ni kuidhalilisha na kuitisha tume isifanye kazi yake .
” Wagombea wa aina hiyo wanapaswa kupuuzwa na watanzania kwani hali hiyo ni moja ya dalili ya uoga anajihami au amekosa sera zakuwaeleza wananchi hivyo hafai kusikilizwa,”amesema Mahera.
Kwa kitendo hicho tume ya maadili taifa imemwandikia barua ya wito Mgombea Urais was CHADEMA, Tundu Lisu, ya kwenda kueleza alichokisema katika kampeni zake alipokuwa mkoani Musoma juzi tarehe 26 hivyo barua hiyo inamtaka aende leo.
Hata hivyo Dk. Mahera amesema kuwa tangu Septemba 25, 2020, Mkurugenzi wa uchaguzi watume ya uchaguzi anaendelea na ziara ya kukagua na kuratibu maandalizi ya uchaguzi katika majimbo ya mikoa ya Manyara, Arusha na Kilimanjaro kuhakikisha vifaa vya uchaguzi Kama vimefika katika maeneo husika.