NA ZUHURA JUMA

TANI 15 zimeteketezwa katika kijiji cha Pujini Wilaya ya Chake Chake Mkoa wa Kusini Pemba baada ya kuonekana haufai kwa matumizi ya binaadamu.

Mchele huo ulikamatwa   ikiwa unabadilishwa na kuwekwa ndani ya vipolo vya Rayyan na Asmin kwa ajili kuuzwa. Kazi hiyo ilikuwa ikifanywa katika ghala la Kizimbani Wete.

Akizungumza baada ya kuteketezwa bidhaa hiyo na bidhaa nyengine, Mkurugenzi wa wakala wa sawa na chakula (ZFDA) Pemba Nassir Salum Bukheti, alisema lengo la kutekeleza bidhaa hizo ni kumlinda mwananchi.

“Leo tupo katika zoezi la kuteketeza bidhaa ya mchele mbovu tulioukamata hivi karibuni pamoja na bidhaa nyengine ambazo tumezipata kutokana na operesheni katika maduka mbali mbali ndani ya mwezi huu wa Disemba,” alisema.

Aidha alielaza bado wanaendelea na msako katika maduka na maghala ambayo yanayohifadhi mchele, ili kubaini iwapo mchele hup uliwahi
kuingizwa kwa ajili ya kuuzwa.
Aliwataka wafanyabiashara na wananchi kwa ujumla
kuhakikisha wanahifadhi vizuri bidhaa za chakula kwenye
maghala na nyumba zao, ili ziwe salama kwa matumizi ya binadamu.

Aliwataka wafanyabiashara hao kuacha udanganyifu kwani wanakwenda kinyume na taratibu, hivyo ikiwa kuna bidhaa imeharibika ni vyema wakaiteketeza.


Mkuu wa idara ya udhibiti  wa ubora wa chakula kutoka
ZFDA, Saade Omar Hamad, alisema mchele huo ulibainika haufai kwa matumizi ya binadamu na ndio sababu wakauteketeza.

Aliwashauri wafanyabiasha wanapochukua bidhaa nyingi waangalie na muda unaotakiwa kukaa kwa ajili ya kusambaza.
Katibu wa sheha shehia ya Pujini Kumvini, Riziki Uledi Kombo, aliipongeza ZFDA kwa kufanya msako katika maduka na kukamata vyakula vilivyoharibika.ya watu.
Nao wananchi walisema kuwa iwapo ZFDA itaendeleza msako katika maduka kwa kutoa vyakula vilivyoharibika itasaidia kuimarisha afya za wananchi.