NA HABIBA ZARALI
WAZIRI wa Uvuvi na Uchumi wa Buluu, Abdallah Hussein Kombo amesema, serikali ya awamu ya nane ina lengo la kuwasaidia wavuvi kujiendeleza kiuchumi.
Aliyasema hayo katika hafla ya kukabidhi boti za doria kwa
baadhi ya kamati shirikishi za usimamizi wa pamoja wa uvuvi jimbo la Mkoani.
Aliwataka wakaazi wa jimbo la Mkoani kudhibiti
uvuvi haramu na kumchukulia hatua yeyote
atakaepatikana akifanya uvuvi haramu.
“La muhimu ni kuzingatia umuhimu wa boti hizi kwa kuzitunza
ili
zidumu na kufaidisha wananchi na sio
vyenginevyo,”alisema.
Ofisa Mdhamini wizara hiyo, Sihaba Juma Vuai,
aliishukuru taasisi ya MCC kwa kuwapatia boti
wavuvi hao ili kulinda rasilimali ya
bahari.
Aidha aliwataka kuwa waadilifu kwani azma ya
serikali ni kuwasaidia wananchi.
Alisema taasisi ya MCC imeanzisha maeneo ya majaribio
kwa
kuanzisha mfuko wa kutunza bahari unaojumuisha
makundi yote ya uvuvi.
Mkurugenzi wa kampuni ya MCC, Ali Khamis Thani,
alisema idara ya uvuvi Zanzibar inafanya kazi na wadau tofauti ikiwemo washirika wa maendeleo
taasisi binafsi kama MCC, mradi wa Swiofish, jamii, serikali za shehia na kamati za uvuvi.
Alisema wanawajengea uwezo wanakamati za uvuvi
katika uendeshaji wa kamati na usimamizi
wa rasilimali za uvuvi ikiwemo mafunzo ya uongozi na utawala bora.
Nao wavuvi hao walishukuru kwa kukabidhiwa boti hizo na
kuitaka wizara ya uvuvi kuwapatia
mafunzo.
Jumla ya shehia nne
zimekabidhiwa boti ikiwemo shehia ya Shidi, Kukuu, Makoongwe na Stahabu.