NA ABUUBAKAR KISANDU
MASHINDANO
ya 15 ya kombe la mapinduzi yamehitimishwa
Jumatano Januari 13, 2021 ambapo Yanga imetwaa ubingwa, baada ya
kuwafunga Simba kwa mikwaju ya penalti 4-3 baada ya dakika 90 kumalizika 0-0 mchezo uliochezwa
saa 2:15 usiku uwanja wa Amaan.
Mara
baada ya kumalizika michunao hiyo kwa mwaka 2021 mwandishi wa Makala hii,
anajaribu kuelezea baadhi ya dondoo kuhusu mashindano hayo.
1.
Yanga ndiyo timu pekee iliyocheza dakika 360 (michezo minne) na kuruhusu mabao
machache (bao moja), ambapo Simba ilicheza dakika hizo (360) na kukubali nyavu
zake kuguswa mara mbili
2.
Simba wanaongoza kucheza fainali mara nyingi kuliko timu yoyote (mara 8)
wakifuatiwa na Mtibwa Sugar (mara 6) ambapo Yanga wamecheza fainali (mara 3).
3.
Simba na Yanga wamekutana mara tatu
katika mashindano hayo zikiwemo mara mbili fainali na mra moja nusu fainali mwaka 2011, walikutana fainali
na Simba wakatwaa ubingwa baada ya kuwafunga Yanga 2-0.
Mwaka
2017 walikutana tena kwenye nusu fainali dakika 90 mchezo ukamalizika kwa
suluhu ya 0-0 na Simba ikashinda kwa Penalti 4-2, lakini mwaka 2021 walikutana
tena katika fainali na Yanga wakashinda kwa penalti 4-3 baada ya dakika 90 kutoka 0-0.
4.
Timu za Zanzibar bado zinaendelea kuwa washindikizaji wa mashindano hayo licha
ya kuwa yanachezwa katika ardhi ya kwao, kwani katika mara 15 zilizochezwa ni
timu moja tu pekee ilitwaa kombe hilo kutoka Zanzibar
ambayo ni Miembeni mwaka 2009.
5.
Mashindano ya mwaka huu Simba imeshinda mabao mengi (mabao 7) ikiruhusu
kufungwa mawili wakati Yanga wakishinda mabao mawili tu na kuruhusu kufungwa
moja.
6.
Kwa mara ya kwanza katika mashindano hayo Simba imemaliza dakika 90 pasipo
kupiga shuti hata moja lililolenga lango
la wapinzani wao Yanga walipiga
mashuti matano yaliolenga lango la
Simba.
7. Miraji Athuman wa Simba ameibuka kuwa
Mfungaji bora akiwa na mabao manne
akiwashinda Meddie Kagere pia wa Simba mwenye mabao mawili na Steven Sey wa Namungo
mabao mawili, ambapo Mkenya Francis Kahata wa Simba amechaguliwa kuwa mchezaji
bora wa mashindano, Mkenya na mlinda mlango wa Yanga Farouk Shikalo ameibuka
kuwa kipa bora, baada lango lake kuruhusu kufungwa bao moja tu katika michezo mine.
Mkenya
Joash Onyango wa Simba alichaguliwa kuwa nyota wa mchezo huo wa fainali, hivyo
kuwafanya wachezaji wa kigeni kutoka Kenya
kutwaa zawadi katika mashindano hayo.
9.
Simba ambayo imecheza fainali nane imeshinda tatu (mwaka 2008,2011 na 2015 na kupoteza 5 (Mwaka
2014,2017,2019, 2020 na 2021) wakati Yanga wamecheza fainali tatu , mbili
wameshinda na moja wamepoteza
(wameshinda 2-1 mbele ya Mtibwa Sugar mwaka 2007 na 2021 wameshinda mbele ya Simba kwa penalti
4-3 baada ya dakika 90 kutoka 0-0 na fainali 1 walifungwa na Simba 2-0 mwaka
2011.
10. Azam FC ndo wanaongoza kubeba mara nyingi (5) walishinda mwaka 2012, 2013, 2017,2018 na 2019 wakiipiku Simba SC ya Dar es Salaam iliyotwaa mara tatu 2008, 2011 na 2015, Mtibwa Sugar mara mbili mwaka 2010 na 2020 na Yanga SC mara mbili 2007 na 2021