Na Mwandishi Wetu, zanzibar

RAIS Samia Suluhu Hassan, ametajwa kutokana na ukomavu wake katika medani za kisiasa, uongozi na utawala atabaki kuwa nguzo  imara kwa hatma na mustakabali utakaodumisha Muungamo wa Tanganyika na Zanzibar .

Pia Rais huyo  wa awamu ya sita amesifiwa akitajwa ni mwenye  mahusiano thabit na mashrika ya kimataifa, mataifa washirika kwa maendeleo aliyejaaliwa ushawishi na mvuto kwa  wawekezaji .

Hayo yamebainishwa jana na Mbunge wa viti maalum  CCM mkoa wa Kaskazini Unguja, Saada Mansour Hussein,  aliyesema hana hofu wala kitete cha  kuyumba Muungano  wa Tanganyika na Zanzibar chini ya uongozi  wa Rais Samia, kwani  anazielewa vyema siasa zake, kero na njia za kufikia utatuzi. 

Saada alisema kiongozi  huyo amepata uzoefu toka akiwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamo wa Rais  Muungano na kabla ya hapo amekuwa Waziri wa Utalii na Uwekezaji SMZ kabla hajawa Naibu spika wa Bunge Maalum la Katiba mahali ambako alipoonyesha ukakamavu wa misuli yake ya ufahamu zaidi   wa siasa na uongozi. 

Alisema kudumu na kuwepo kwa muungano imara wenye usawa na heshima, ni uhakika na usalama kwa ustawi wa maisha ya watu na mali  zao, kuendeleza udugu , kuimarika biashara na ,masoko ,  kuendelea kwa ushurikiano huku taifa likibaki moja bila kugawanyika.

“Tumempata mrithi sahihi wa kiti cha Urais  mwenye uwezo, upeo  na ufahamu. Ni kiongozi  makini ,hodari na mchapakazi. Amepata uzoefu na kukomaa kisiasa na kiutawala.Rais samia atakuwa  nguzo imara kwa mustakabli na hatma ya  muungano wetu “Alisema  Saada.

Aidha Mbunge huyo alisema kiongozi mwanamke aliyepata nafasi ya kuwa Rais awanu ya sita alimtaja ni  mtulivu ,msikivu na mvumilivu kwani hupendelea kuendesha mambo kwa njia ya majadiliano kwa hoja mezani hadi kufikia tamati na muafaka kwani haamini kama jazba na pupa huleta suluhisho .

Kadhalika Mbunge huyo aliwataka wanawake wote nchini bila kujali vyama vyao sasa waweke pembeni tofauti zao za kisiasa na kuona huu ni wakati muhimu kwa wanawake wote kusimama pamoja na kuanza kuvuta  kamba ya umoja na ushirikiano.

‘Wanawake wote duniani  walipambana kupinga mifumo yote dume iliokandamiza haki za wanawake .Haitawezekana kila mwanamke  ashike nafasi ya juu kwa wakati  mmoja. Mwenzetu au kuwa wabunge .Mmoja anapofanikiwa ihesabike huo ni ushindI wa wanawake wote nchini  “Alisisitiza saada 

Vile vile alisema kwa miaka mingi  duniani ilimuona mwanamke ni mtu wa mwisho anayestahili kukosa haki 

Ilitosha ababaki nyumbani, akionekana ni nyenzo ya  uzalishajimali katika kila familia akiwa kama mhudumu wa familia huiu akizalishwa bila kufuata uzazi wa mpango na uzazi  salama.