NA VICTORIA GODFREY

TIMU ya Tambaza Youth  imeibuka na ushindi wa mabao 2-1 dhidi  ya Boom katika mashindano ya Jiandae Cup wilaya ya Ilala uliochezwa juzi kwenye dimba la Airwing,Dar es Salaam.

Dakika ya 21 Devis Emmanuel wa Tambaza alifunga bao la kwanza na  Salim Ndodi aliongeza  la pili dakika ya 32, Boom ilipata bao la kufutia machozi  kipindi cha lala salama kupitia Khalid Khalid dakika ya 89.

Katibu Mkuu wa Chama cha Soka Wilaya ya Ilala (IDFA) Daud Kanuti, alisema mashindano yanakwenda vizuri na ushindani mkubwa.

Alisema timu zote zimecheza vizuri kila mmoja apate matokeo mazuri na hilo limewezekanana kupata mshindi wa mchezo huo.

” Niwapongeze timu zote mbili kwa  kuonyesha mchezo mzuri na wa ushindani kwani tunaimani malengo yetu yatatimia kwa timu  kuwa imara katika ligi zijazo.

Alisema malengo ni kuwaandaa wachezaji na makocha kupata nafasi ya kubaini kasoro ambazo watazifanyia kazi  waonyeshe ushindani katika ligi daraja la Tatu na  Nne .