FLORIAN NEUHAUS

LIVERPOOL inafanya mazungumzo na Borussia Monchengladbach ili kumsajili kiungo wa Ujerumani Florian Neuhaus, 24. (Sport1 – in German)

PAULO FONSECA

MENEJA wa zamani wa Roma Paulo Fonseca amekubali kimsingi mkataba wa miaka miwili kuinoa Tottenham. (Telegraph)

BEN WHITE

ARSENAL wanaandaa mpango wa kumsajili beki wa kati wa Brighton na England Ben White, 23. (Athletic)

MANUEL LOCATELLI

GUNNERS pia wanamtazama kiungo wa kati wa Italia mwenye umri wa miaka 23 Manuel Locatelli. (Sky Sport Italia, via Metro)

Jadon Sancho

WINGA wa Uingereza Jadon Sancho, 21, atakuwa mshindi wa pili kwa juu Manchester United, nyuma ya kipa David de Gea, ikiwa atakamilisha uhamisho kutoka Borussia Dortmund msimu huu wa joto. (Mail)

SERGIO RAMOS

SEVILLA wamempa mlinzi wa kati wa Uhispania Sergio Ramos, 35, mkataba wa miaka mitano. Ramos amemaliza mkataba na Real Madrid msimu huu wa joto. (esRadio – in Spanish)

SAUL NIGUEZ

CHELSEA inavutiwa na kiungo wa Atletico Madrid Saul Niguez, 26, lakini Manchester United na Juventus wanabaki kuwa vipenzi vya kumsajili mchezaji huyo wa Uhispania. (Mundo Deportivo – in Spanish)

ROBERT LEWANDOWSKI

MSHAMBULIAJI wa Poland Robert Lewandowski, 32, yuko tayari  kuondoka Bayern Munich. (AS – in Spanish)

NIKOLA VLASIC

EVERTON wanafikiria kumsajili tena mshambuliaji wa Croatia Nikola Vlasic, 23, kutoka CSKA Moscow – miaka miwili baada ya kumuuza. (Star)

SERGE AURIER

BEKI wa kulia wa Tottenham na Ivory Coast Serge Aurier, 28, amekubaliana masharti ya kibinafsi na Paris St-Germain. (Football Insider)

DANNY ROSE

MLINZI wa pembeni wa England Danny Rose, 30, anakaribia kujiunga na Watford baada ya kuondoka Tottenham. (Watford Observer)

GIANLUIGI DONNARUMMA

MLINDA mlango wa Italia Gianluigi Donnarumma, 22, anakaribia kukamilisha uhamisho wa bure kwenda Paris St-Germain. Ataondoka AC Milan msimu huu wa joto wakati mkataba wake utamalizika. (Calciomercato – in Italian)