ZASPOTI
NYOTA wa Senegal, Idrissa Gueye, anafurahia kupitia uzoefu wake kwa vijana katika klabu yake ya Ufaransa ya Paris Saint-Germain katika michezo yao ya kirafiki ya maandalizi ya msimu.
Kiungo huyo mwenye uzoefu ameiongoza miamba hiyo ya ‘Ligue 1’ kama nahodha katika mechi zao tatu za mwisho huku nahodha wa klabu, Marquinhos, akiwa yuko likizo baada ya kuichezea Brazil kwenye michuano ya Copa America 2021.
Chini ya unahodha wa Gueye, PSG ilipata ushindi wa magoli 4-0 dhidi ya Le Mans kabla ya kushikiliwa kwa sare ya 2-2 na Chambly na Paris walitangaza ushindi wa 2-1 dhidi ya klabu ya Bundesliga ya Augsburg.
“Ni wazi nina furaha, na vijana hawa ambao wanatuheshimu na wanasikiliza”, Gueye aliiambia tovuti rasmi ya klabu.
“Ni muhimu kwangu kupitisha uzoefu wote ambao nimekusanya wakati wa kazi yangu.
“Ukweli tu wa kuwabadilisha vijana, ukweli wa kuweza kujadiliana nao, kuwaonyesha mfano wa uhakika na nje ya uwanja, ni raha tu kwangu.”
Gueye, ambaye amekuwa kwenye vitabu vya PSG tangu 2019, anaamini timu hiyo ipo kwenye njia sahihi na kampeni mpya itakayoanza mwezi ujao.
Nyota huyo mwenye umri wa miaka 31 amefunga magoli matano kwenye mechi 78 za kimataifa akiichezea Senegal.(AFP).