NA TUWERA JUMA ‘MCC’

NAIBU Katibu Mkuu  Mufti wa Zanzibar, Fahim Hafidh Hassan amewataka waumini wa dini ya kiislamu kujitokeza kwa wingi   kusajili madrasa na miskiti iliyopo katika shehia zao.

Aliyasema hayo huko ofisini kwake Mazizini wakati alipokuwa akizungumza na gazeti hili alisema watu watakapo  jitokeza itawaondoshea usumbufu  pale wanapotaka kutoa elimu.

Alisema kufanya hivyo itawapa wepesi pale panapotokezea misaada mbali mbai kutoka sehemu tofauti, kwani itakuwa  rahisi wa kuzitambua  zinapo patikana na kuwa na takwimu sahihi .

Alifahamisha kuwa  usajili unasaidia kupata haki zako zote kutoka serikalini ,ukitaka kufunguwa  benki akauti itakulazimu uwe na usajili, pamoja na kuomba misaada kutoka nje .

Alisema jumla ya miskiti iliyopo Unguja ambayo tayari imeshasajiliwa  ni 1,775 , na madrasa za  Unguja 1,893 na kwa upande  miskiti 2,870 na madrasa 4,947 .

Alisema wanampago maalum wakuanzisha hapo  badae wa kuweka  misikiti na madrasa kama mfumo wa skuli na walimu watakuwa wale ambao waliopatiwa mafunzo maalumu yanayotolewa katika ufisini kwao.

“Wito wangu kwa waumini wazangu wa dini ya kislamu wajitokeze kwa wingi kuja kuzisajili madrasa na misikiti ambayo ipo katika shehia zao ili waunge mkono juhudi za serikali ya awamu ya nane “alisema Fahim.