ZASPOTI
Fode Ballo-Toure
BEKI, Fode Ballo-Toure, alitarajiwa kuwasili Italia juzi kukamilisha uhamisho wa kwenda AC Milan.
Lakini, mipango ya matibabu yake imefutwa, kulingana na Gianluca Di Marzio kwani miamba hiyo ya ‘Serie A’ bado unahitaji kufikia makubaliano na Monaco na kupata maelezo kamili ya mpango huo. (Goal).
Anton Kresic
KIUNGO, Anton Kresic amejiunga na klabu ya Rijeka kwa mkopo, Atalanta alithibitisha.
Kresic alitumia misimu miwili iliyopita kwa mkopo huko Padova na sasa atatumia kampeni ya 2021-22 huko Croatia.(Goal).
Andriy Yarmolenko
KLABU ya West Ham na Fenerbahce wapo kwenye mazungumzo juu ya dau la pauni milioni mbili kwa ajili ya Andriy Yarmolenko.
Nyota huyo wa Ukraine alijiunga na timu hiyo ya Ligi Kuu ya England akitokea Borussia Dortmund miaka mitatu iliyopita na huenda akaendelea na maisha yake Uturuki.(Insider).
Soualiho Meite
KIUNGO, Soualiho Meite anajiandaa kujiunga na Benfica.
Nyota huyo mwenye umri wa miaka 27 alitumia msimu uliopita akiwa mkopo AC Milan na ataondoka Torino kwa dau la kudumu, huku klabu hiyo Ureno ikiwa tayari kulipa Euro milioni saba.(Record).
Willian Jose
REAL Sociedad inataka dau la euro milioni sita kwa ajili ya Willian Jose.
Mshambuliaji huyo ni mlengwa mkuu wa Besiktas ya Uturuki na wakati wapo tayari kuridhia bei hiyo ya kuuliza, ingawa wanataka kutoa malipo kwa zaidi ya miaka minne. (Mundo Deportivo).
Lorenzo Insigne
NAPOLI wanasubiri kwa hamu kurudi kwa Lorenzo Insigne kutoka likizo ili waweze kuanza kujadili mkataba mpya.
Mkataba wa nyota huyo wa Italia unamalizika kiangazi kijacho, lakini, Corriere dello Sport linasema klabu hiyo ya ‘Serie A’ inatarajia kumshawishi kuongeza muda wa kubakia kwake hivi karibuni.(Corriere dello Sport).
Nuno Espirito Santo
KOCHA, Nuno Espirito Santo, amethibitisha Gareth Bale hatarejea Tottenham kwa kampeni ya 2021-22.
Hatma ya Bale bado haijaamuliwa kwani kulikuwa na uvumi kwamba angeweza kurejea London kaskazini kwa kampeni ya 2021-22, wakati ilidaiwa pia kuwa anaweza kustaafu. (Goal).
Monchu
KIUNGO, Ramon Rodriguez ‘Monchu’ amejiunga na Granada akitokea Barcelona.
Monchu amefaulu vipimo vya afya na amethibitishwa kama usajili wa hivi karibuni wa klabu hiyo ya Ligi Kuu ya Hispania.(Goal).
Pierluigi Gollini
KLABU ya Tottenham inamtaka mlinda mlango wa Atalanta, Pierluigi Gollini.
Miamba hiyo ya Ligi Kuu ya England inazungumza na upande wa ‘Serie A’ juu ya mkataba wa mkopo na jukumu la kununua moja kwa moja.(Sky Sport).
Alex Telles
KLABU ya Inter Milan inaangalia kumsaini, Alex Telles kwa mkopo.
Telles hapo awali alichezea klabu hiyo kwa mkopo mnamo 2015-16 na anaweza kufurahia kurejea kwenye timu hiyo ya Italia. (Goal).