MABAO matatu aliyofunga Bruno Fernandes yamemfanya kuwa mchezaji wa bora wa mechi ya ligi kuu Uingereza, ambayo Manchester United walishinda mabao 5-1 dhidi ya Leeds.
Mchezo huo wa ligi kuu England ulipigwa katika dimba la Old Trafford wiki iliyopita, lakini Paul Pogba alionekana kuwa mwenye msaada kwenye mechi hiyo.
Kwa kipindi sasa hakukuwa na mjadala kuhusu ubora wa Fernandes ndani ya Old Trafford tangu ajiunge akitokea Sporting Lisbon Januari, 2020, huku kwa Pogba pengine ndio matumaini yapo tofauti zaidi.
Siku ya Jumamosi jina la Graeme Souness lilionekana kuvuma zaidi ikiwa ni moja ya ujumbe kwa nyota huyo wa zamani wa Liverpool na Scottland ambaye ametumiwa kama mfano baada ya msaada aliokuwa akiutoa Pogba kwenye mechi hiyo.
Katika utafutaji wa mabao matano, jina la Pogba limeingia kwenye orodha ya wachezaji saba, ambao walionekana kuwa na msaada mkubwa katika mechi ndani ya ligi kuu ya Uingereza, na hii inamfanya kuwa mchezaji wa kwanza akitokea Manchester United , msaada wa Harry Kane uliopelekea mabao 5-2 dhidi ya Southampton Septemba 2020.
“Watu wanazungumzia ubora wa Paul,” Amesema Fernandes, “lakini ubora wake haujadiliwi. Tunafahamu fika anachokifanya na umuhimu wake.
“Paul ni mchezaji mwenye umuhimu mkubwa kwetu. Ili tupate ushindi kama wa leo tulimhitaji sana.”
Ni jambo la kushangaza kwamba katika mchezo mmoja Pogba ameweza kuweka tofauti ya kimahesabu ya kuisaidia timu ukilinganisha na mechi tatu za msimu wa uliopita.
Pasi ya kwanza ya wazi aliyopewa Fernandes ilikuwa ngumu kutafsiriwa na Pascal Struijik na kumfikia Mason Greenwood, pasi fupi kwa Fernandes alioutoa kwa mguu wake wa kushoto kueleke kwa Fred katika nafasi ya kukamilisha mzunguko wao.
Mchanganuo wa mchezo mmoja unamuweka Pogba juu kwenye orodha ya wachezaji wenye ushawishi mkubwa ulimwenguni.
Tatizo ni kwamba licha ya kufikia viwango hivyo, bado raia huyo wa ufaransa ameonekana kuwa hawezi kuwa na mchango zaidi kwenye mechi.
Ndio maana kumeonekana kuwepo kwa mazungumzo mengi katika majira ya joto kama wangemuuza mchezaji huyo, ambaye aliingia Manchester United kwa dau la pauni milioni 89 akitokea Juventus mwaka 2016 – kwa mara ya pili – huku mkataba wake ukisalia mpaka kipindi kijacho cha joto.
Ama Pogba ataondoka msimu ujao wa joto kama mchezaji huru-wakala wake Mino Raiola alitumia mbinu hiyo hiyo kwa mchezaji Gianluigi Donnarumma msimu uliopita, aliondoka AC Milan kwenda PSG – au atasaini nyongeza ya faida na kukaa na Manchester United.
Kocha wa Manchester United Ole Gunnar Solskjaer ameonekana kuchoshwa na mazungumzo, yanayomhusu mchezaji huyo licha ya kwamba alifuatwa mara mbili, katika mkutano wake na waandishi wa habari alijaribu kukimbia maswali na kubainisha kuwa kwa sasa anaangalia kwa undani namna kikosi chake kinavyocheza.
“Paulo ana maono na ameonyesha viwango bora zaidi,” alisema. “Nimevutiwa sana na viwango vyake sanjari na utayari wake pia. Anaonekana yuko tayari kusonga nasi.
“Miezi 18 iliyopita imekuwa ya kushangaza – mwingiliano pekee umekuwa kupitia vyombo vya habari na kutazama mechi kwenye runinga, ili kurudisha umoja wetu kwa mashabiki.
Hii ndio Manchester United halisi. Hivi ndivyo nilivyoiwezesha timu kupitia Edinson Cavani na akasema huwezi kuondoka baada ya msimu mmoja bila mashabiki. Kujibu swali lako ‘ndio’. ”
Swali ni Je? Mashabiki wanaorudi wanaweza kuwa wanafanya kumshawishi Pogba kusalia klabuni hapo.
Inaweza isiwe sababu mojawapo, Fedha iliyowekwa huenda ndio inaweza kumaliza mazungumzo ya mchezaji huyo mwenye miaka 28 na kuamua kitakachotokea hapo baadae.