NA NASRA MANZI, WHVUM
WAZIRI wa Habari Vijana ,Utamaduni na Michezo, Tabia Maulid Mwita, amesema Serikali kupitia Wizara hiyo imetenga fedha Shilingi bilioni saba kwa ajili ya vijana kujiwezesha wenyewe.
Akizungumza mara baada ya matembezi yaliyoambatana na mazoezi ya umoja wa Vijana Mkoa wa Mjini (UVCCM) yaliyoanzia Aman hadi katika viwanjan vya maisara KMKM Mjini Unguja.
Alisema lengo la serikali kutenga bajeti hiyo, ni kuwawezesha vijana katika shughuli mbali mbali za kujiinua kiuchumi na kupata maendeleo.
Aidha, aliwataka vijana kuchangamkia fursa na kutochagua kazi ya kufanya, kwani Serikali imetenga bajeti, ili kuwainua kiuchumi na kupunguza malalamiko.
Alisema Wizara pia imejipanga vyema namna ya kubuni miradi na kuwawezesha vijana pamoja na mabaraza mengine, ili kufanya biashara ,Sambamba na kuwatafutia soko kwa lengo wanachozalisha kuleta tija kwa kuepusha upotevu wa fedha na kuepusha kuitia hasara serikali.
Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana Mkoa wa Mjini Kamaria Suleiman, alisema wataendelea na mazoezi katika kuhakikisha umoja vijana UVCCM unakua imara na kujenga Afya zao.
Alisema agizo hilo la kufanya mazoezi kutoka kwa Katibu Mkuu UVCCM Taifa, litakuwa endelevu na kuwafanya Vijana kufanya Kazi kwa umoja na mshikamano katika majukumu yao.