NA NASRA MANZI, WHVUM

WAZIRI wa Habari,Vijana Utamaduni na Michezo Tabia Maulid amesema ujio wa viongozi wa mpira wa miguu kutoka Misri, umeahidi kuwekeza Zanzibar, katika michezo ili kuwapatia fursa na kunyanyua soka nchini.

Akizungumza na ugeni huo baada ya kuwasili ofisi za Wizara ya Habari,Vijana,Utamaduni na Michezo huko Migombani Mjini Unguja.

Alisema ujio huo utafungua milango na fursa za michezo kwa vijana pamoja na fursa nyengine za kuekeza katika utalii, kwa kisiwa cha Unguja na Pemba  ili kuongezeka kwa wageni .

Tabia alieleza wameahidiana  kurejesha utamaduni uliopo zamani kwa timu ya Taifa ya Zanzibar kwa kukaaa kambi nchini Misri kwa lengo la kupata uzoefu na mazoezi zaidi.

“ Viongozi wa mpira wa miguu  kutoka Misri wametuahidi mambo mengi ya kutuletea maendeleo nchini kwetu,  tumefarajika kama wizara, lakini pia serikali yetu ya awamu ya nane imetilia mkazo masuala ya michezo ,uwekezaji na kukuza utalii “ alisema

Alisema serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar itaendelea kushirikiana na  kudumisha  mahusiano na serikali ya nchini  Misri , kwa kutekeleza ilani na kumsaidia Rais wa Zanzibar Dk. Hussein Mwinyi  katika kukuza mahusiano na nchi jirani.

Nae Mtendaji Mkuu (CEO) kutoka Kampuni ya Captex kutoka Misri  Mohamed Hassan Abouzeid, alisema wapo tayari kuendelea kushirikiana na Zanzibar, katika kuimarisha na kukuza  michezo ,pamoja na kuwekeza ili kuona mpira wa  miguu Zanzibar unapiga hatua.

Aidha serikali ya Misri imeahidi pia kutoa vifaa vya michezo na  uwekezaji na kuwekeza sehemu nyengine za utalii.

Nae Rais wa Chama Cha mpira wa miguu Zanzibar  Abdulllatif Ali Yassin ametoa wito kwa wanamichezo nchini, husuan mpira wa miguu kuitumia fursa hiyo kwa  wawekezaji hao  kutoka nchini Misri , kwani  wana lengo la kuwekeza katika soka la vijana sambamba na   kuuza wachezaji nje ya nchi na pia kuimarisha viwanja na Academy