WAPENZI wasomaji wetu wa Zanzibar Leo Jumapili, leo katika safu hii ya maakuli lnimewatayarishia upishi mwanana wa vitumbua vya kuku.

Jaribu leo hii na uone namna upishi huu ulivyo mtamu kwani wengi wamezuea kupika vitumbua vya nyama yam ng’ombe.

Hivyo wikiendi hii ni bora kubadilisha na kupika vitumbua hivi na utaona mabadiliko yake kwa namna familia itakavyopenda upishi huu.

Basi fuatilia namna ya mahitaji yanayotakiwa, vipimo na namna ya kupika vitumbua vya nyama ya kuku.

VIPIMO

Kuku – 3 Lb

Mayai – 6

Baking Powder – 1 kijiko cha chai

Pilipili boga – Robo kipande

Kitunguu maji – 1 kidogo

Pilipili manga ya unga – 1 kijiko cha chai

Kitunguu saumu(thomu) na Tangawizi – 1 kijiko cha supu

Chumvi – ½ kijiko cha chai

Mafuta ya kuchomea

NAMNA YA KUTAYARISHA NA KUPIKA

  1. Chemsha kuku  mpaka awive. hakikisha umemchemsha na viungo vyote. baada ya kuwiva,  toa mifupa kwa kunyambua mnofu vipande vidogo vidogo.
  2. Kata kitunguu  vipande vidogo vidogo
  3. Kata pilipili boga (la kijani) vipande vidogo
  4. Tia vitu vyote hivyo katika mashine  la kusagia (Blender)
  5. Tia mayai, hakikisha mayai yanafunika mchanganyiko.
  6. Saga kwa muda mfupi tu.
  7. Weka mchanganyiko  uliosagika vizuri kwenye bakuli.
  8. Tia chumvi, pilipili manga na baking powder.
  9. Tayarisha chuma  cha kuchomea vitumbua kwenye jiko.
  • Weka mafuta kidogo.
  • Choma kama unavyochoma vitumbua vya mchele.