Skip to content

Miundombinu ya kisasa  itaharakisha  upatinajaji haki – Dk. Shein

  • Zanzibar

RAIS mstaafu wa Zanzibar wa awamu ya saba, Dk. Ali Mohamed Shein amesema Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar itaendelea kuimarishamiundombinu ya kisasa inayohakikisha wananchi wanapata haki zao kwa mujibu wa sheria.

Ameeleza hatua hizo ni pamoja na kujenga majengo ya kutosha ili kesi   zinazowasilishwa mahakamani zipate nafasi ya kuendeshwa na kutolewa mamuzikwa haraka zaidi  ili kupunguza mrundikano.

Dk. Shein alieleza hayo wakati wa ufunguzi wa jengo la mahakama ya mkoa wa Kaskazini Unguja huko pale na kuongeza kuwa hapo awali mahakama ilikuwa na majengo finyu yaliyosababisha kuchelewa kutolewa kwa maamuzi hivyokuchelewesha upatikanaji wa haki kwa wananchi.

Aidha rais huyo mstaafu alieleza kuwa inapendeza kuona sasa kuna majengomazuri na yenye nafasi pamoja na vitendea kazi watu jambo litakalochochea kasiya upatikanaji wa haki kwa wakati.

“Huu ni ushahidi kwamba Zanzibar ni nchi inayoheshimu utawala wa sheria inayojengwa kwa kuwepo mihimili mitatu ya serikali, Baraza la Wakilishi na Mahakama  ambayo ni misingi muhimu duniani katika utekelezaji wa utawalabora”, alieleza Dk. Shein.

Aidha Dk, shein aliwataka wananchi kutumia mahakama kutoa ushahidi pale wanapohitajika ili kusaidia kupatika kwa haki kwani ushahidi ndio unaopelekeamtu kupata haki hivyo wananchi wasihofie.

Vile vile aliwataka Majaji na Mahakimu kufuata sheria na kutoa haki kwa wananchi kwani jambo la haki limetajwa hata nadani ya vitabu vitukufu vya dini hivyo wanapaswa kuwa waadilifu.

Naye Mtendaji Mkuu wa mahakama, Kai Bashir Mbarouk, akisoma ripoti  ya kitaalamu juu ya ujenzi huo , alisema serikali ya awamu ya nane iliamua kujengamajengo saba ya mahakama kwa mikoa na wilaya zote za Zanzibar yanyojengwakwa awamu ambapo jengo hilo ni  miongoni mwa majengo hayo.

Aidha Kai alifahamisha kuwa gharama za ujenzi huo  na majengo mengineyaliyojengwa yamegharimu shilingi 28 fedha zilizotolewa na serikali ambapo hadisasa zaidi ya shilingi bilioni 14 zimelipwa huku ujenzi huo ukifikia asilimia 83.

Aliongeza kuwa jengo hilo la ghorofa moja lina vyumba vyote vya kimahakama ofisi za Majaji, Mahakimu, Makadhi na watendaji wote wa mahakama wakiwemoMawakili waserikali na kujitegemea, ofisi za wasaidizi wa sheria, jeshi la polisichuo cha mafunzo, sehemu ya kuhifadhiwa watuhumiwa na kumbi za kusikiliziamashauri uzinazozingatia usalama na watu wenye mahitaji malum.

Mapema Mkuu wa mkoa wa Kaskazini Unguja, Matar Zahor Masuod, akimkaribisha mgeni rasmi  alisema  mapinduzi yamekuja kumkomboa mnyongekwa kuleta haki na fursa  kutokana na mateso waliyokuwa wakiyapata wakati wa ukoloni.

“Lakini leo tunashukuru kuona kuwa mkoa wetu umechukuwa nafasi pana kwa uzinduzi wa majengo ya maendeleo likiwemo jengo hilo la mahakama kwanimaendeo haya ni matokeo ya kazi kubwa iliyofanya na wazee wetu waliofanyaMapinduzi”, alieleza Mattar.

Kilele cha maaadhimisho ya miaka 61 ya Mapinduzi kinatarajiwa kufanyika katikauwanja wa gombani pemba ambapo kuanzia Disemba 20, mwaka huu viongozimbali mbali wa kitaifa wamekuwa wakizindua, kukagua na kuweka mawe ya msingi wa miradi ya maendeleo katika sekta mbali mbali.