Skip to content

TANESCORuvuma kufikisha huduma ya umeme kila kitongoji

  • Bara

NA STEPHANO MANGO, SONGEA

SHIRIKA la Umeme Tanzania, TANESCO, mkoa waRuvuma, limesema litahakikisha kila mwananchi wa mjinina vijijini anafikiwa na huduma ya umeme  ili kuongezamatumizi ya nishati safi ya kupikia.

Akizungumza na wakazi wa mkoa wa Ruvuma, Zachariah Julius Stephano kutoka TANESCO, aliwahimiza wananchikujijengea utaratibu wa kutumia nishati safi ya kupikia kwagharama nafuu na salama.

Alisema watu wasihofu kutumia nishati safi ya kupikiakama vile majiko ya umeme na vifaa vyote vya mapishivinavyotumia umeme.

Badala yake alisema watumie kwa wingi kwani vifaa vyotevimetengenezwa kutumia kiwango kidogo cha umemeambapo uniti moja ya umeme mteja anaweza kupikachakula cha familia.

Kwa upande wake, Mhandisi wa mita za luku, Brown Mkole, aliwataka wateja wa TANESCO kuwa na utaratibuwa kufanya ukarabati wa miundombinu ya nyaya zaumeme kila baada ya miaka 10 ili kujihakikishia usalama.

Alisema kama mteja anapata changamoto ya matumizi yaumeme kuwa juu tofauti na kiwango anachodhaniametumia, ajitahidi kutoa taarifa ili kuwasaidiwa.