Skip to content

Urusi inatumia ‘warembo’ kufanya ujasusi Marekani

  • Makala

Katika miaka ya hivi karibuni hata hivyo mashirika ya kijasusi ya Marekani yamefaulu kuvunjamitandao ya siri ya oparesheni za kijasusi za Urusi nchini mwao.  

Taarifa zinaonesha kuwa Urusi inatumia wanawake warembo kupindukia ambao walipewamafunzo maalum waliotumiwa kwa miaka mingi katika oparesheni hizo za Moscow.

Unaweza kusema walitoka ‘Moscow na mapenzi’ kumbe walikuwa na hila. Hawa hapa baadhi ya wanawake kama hao waliokamatwa kwa kushukiwa kuwa majasusi wa Moscow.

Maria Butina: Mnamo mwezi Julai mwaka wa 2018, serikali ya Marekani ilitangaza kumkamatamwanamke mwenye umri wa miaka 29 raia wa Urusi kwa jina Maria Butina.

Alishtumiwa kwa kuifanyia kazi serikali ya Urusi na lengo lake lilikuwa kuyaingilia makundi ya kisiasa nchini Marekani kwa lengo la kupata habari zinazoeza kutumiwa kuihujumu Marekani.

Maria Butina alianzisha uhusiano wa karibu na chama cha Republican na alikuwa mtetezi wa haki za kumiliki bunduki, kulingana na ripoti za vyombo vya habari nchini Marekani.

Mashitaka dhidi yake hayakuhusiana na uchunguzi wa jopo la Mueller ambao ulihusu madai ya Urusi kuingilia uchaguzi wa Marekani wa mwaka 2016. Mwanadada huyo inasemekana alifanyakazi kwa maelekezo ya maofisa wa ngazi za juu wa Kremlin.

Wakili wa Butina, Robert Driscoll alisema kwamba mteja wake alikuwa sio jasusi na badalaalikuwa mwanafunzi wa uhusiano wa kimataifa ambaye alilenga kutumia digrii yake kufanyataaluma ya biashara.

Butina aliingia Marekani kama mwanafunzi ni mzaliwa wa Siberia na alikwenda Marekani kwa visa ya mwanafunzi kusoma katika Chuo Kikuu cha Amerika. Malalamiko hayo yanadaikwamba alikuwa akiifanyia kazi kwa siri serikali ya Urusi.

Alianzisha kikundi kinachoitwa ‘Right to Bear Arms’ kabla ya kufika Marekani, na vyombo vyahabari vya Marekani hapo awali viliripoti uhusiano wake na chama cha kitaifa cha Bunduki(NRA), kundi lenye uhawishi mkubwa kuhusu haki ya kutumia nguvu ya bunduki nchini Marekani.

Hapo awali alikanusha kufanya kazi na serikali ya Urusi, hata hivyo gazeti la Washington Post iliripoti kwamba alikua msaidizi wa benki ya Urusi na seneta wa zamani Alexander Torshin.

Pages: 1 2 3