Skip to content

Dk. Mwinyi: Mazoezi kinga madhubuti ya maradhi

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Hussein Ali Mwinyiamewataka wananchi wa Zanzibar kuendelea kufanya mazoezi kwani ni kinga madhubutidhidi ya maradhi hasa yasioambukiza.

Dk. Mwinyi aliyasema hayo katika viwanja vya Mnazimmoja Wete wakati akizungumza nawananchi waliojikeza katika bonanza la mazoezi kitaifa lililoambata na na matembeziyaliyoanzia katika uwanja wa mpira Kinyasini hadi uwanja wa Mnazimmoja, Wete Pemba.

Alieleza kuwa kufanya mazoezi kutaweza kupunguza na kuondosha maradhi yasioambukizayakiwemo ya kisukari, presha pamoja na unene uliyokithiri.

Aidha Dk. Mwinyi alifahamisha kuwa kuwa maradhi yasioambukiza yamekuwa yakiongezekasiku hadi siku yakilinganishwa na maradhi yanayoambukiza ambayo yalikuwa yakiongoza katikamiaka iliyopita.

“Niwaombe sana ndugu wananchi, tusiache kufanya mazoezi kwani kufanya mazoezikunapelekea kujikinga na maradhi yasioambukiza,  hili tuelewe wazi”, alieleza Dk. Mwinyi.

“Lakini pia niwafahamishe wana michezo wenzangu kuwa mazoezi ni afya, hivyo tuendeleekufanya mazoezi ili tuweze kuweka miili yetu sawa”, alieleza Dk. Mwinyi.

Sambamba na hayo Rais Mwinyi aliwataka wananchi wa Zanzibar kuendelea kudumisha hali ya amani, umoja na utulivu uliopo nchini hasa katika kipindi hiki nchi ikielekea katika uchaguzimkuu hapo baadae.

“Niwaombe sana viongozi wa dini na wanasiasa kuendelee kuwahubiria wafuasi wetu juu ya umuhimu wa kuitunza amani ya nchi iliyopo”, alisisitiza Dk. Mwinyi. 

Mapaema Dk. Mwinyi aliupongeza uongozi wa Chama cha Wafanya Mazoezi Zanzibar (ZABESA) kwa kuwashajihisha wananchi kuendelea kufanya mazoezi pamoja na kuendelezasiku ya mazoezi kitaifa nchini.

Aidha Rais Mwinyi alivipongeza vikundi vyote vya mazoezi pamoja na wananchi wotewaliojitokeza katika kushiriki bonanza hilo kwa mwaka huu.

Naye Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar, Lela Muhamed Mussa akizungumza kwa niaba ya Waziri wa Habari, Utamaduni na Michezo Zanzibar, Tabia Maulid Mwita, aliahidikuendelea kuondoa changamoto zote zinajitokeza katika bonanza hilo kila mwaka.

Lela pia alimpongeza Rais Dk. Mwinyi kwa hotuba yake aliyoitoa kuuaga mwaka 2024 na kuukaribisha mwaka mpya wa 2025 na kueleza kuwa hotuba hiyo inafaa kuwekwa katika kitabumaalum kwani imeonesha dhahiri imani ya Rais ni kubwa kwa wananchi wake.

“Nikuahidi kuwa tutashirikiana kwa pamoja ili kuhakikisha amani,Umoja na Utulivu ulioponchini tutaweza kuuendeleza kwa hali zote” alisema Waziri Lela.

Katika bonanza hilo vikundi vya mazoezi kutoka Unguja, Pemba na Tanzania bara vipatavyo 18 vilihiriki kwenye bonanza hilo la 10 toka lilipoasisiwa linalofanyika kila januari 1 ya kila mwaka.